Saturday, May 5, 2012

Change the Way You Think about Money for a good start,What people don't realize is that entire armies are built one soldier at a time


Change the Way You Think About Money for a good start
The general population has a love or hate relationship with money. They resent those who have it, but spend their entire lives attempting to get it for themselves. The reason majority of people never accumulate a substantial nest egg is because they don't understand the nature of money or how it works.
Cash, like a person, is a living thing. When you wake up in the morning and go to work, you are selling a product - yourself (or more specifically, your labor). When you realize that every morning your assets wake up and have the same potential to work as you do, you unlock a powerful key in your life. Each dollar you save is like an employee. Over the course of time, the goal is to make your employees work hard, and eventually, they will make enough money to hire more workers (cash). When you have become truly successful, you no longer have to sell your own labor, but can live off of the labor of your assets.
Develop an Understanding of the Power of Small Amounts

The biggest mistake most people make is that they think they have to start with an entire Napoleon-like army. They suffer from the "not enough" mentality; namely that if they aren't making $1,000 or $5,000 investments at a time, they will never become rich. What these people don't realize is that entire armies are built one soldier at a time; so too is their financial arsenal.
A woman who worked as a dishwasher and made her purses out of used liquid detergent bottles. This woman invested and saved everything she had despite it never being more than a few dollars at a time. Now, her portfolio is worth millions upon millions of dollars, all of which was built upon small investments. I am not suggesting you become this frugal, but the lesson is still a valuable one. Do not despise the day of small beginnings!
With Each Dollar You get, You Are Buying Yourself Freedom
When you put it in these terms, you see how spending $20 here and $40 there can make a huge difference in the long run. Since money has the ability to work in your place, the more of it you employ, the faster and larger it will grow. Along with more money comes more freedom - the freedom to stay home with your kids, the freedom to retire and travel around the world, or the freedom to quit your job. If you have any source of income, it is possible for you to start building today join now click here to learn more on how you can built your own from scratch it takes a little time start now 

Friday, May 4, 2012

RAIS JAKAYAKI KWETE AKITANGAZA BARAZA LA MAWAZIRI



















Rais Jakaya Mrisho Kikwete 
akiongea na Makamu wa Kwanza wa Rais 
Dkt Mohamed

 Gharib Bilali na Waziri Mkuu Mh Mizengo
Pinda baada ya kutangaza 
Baraza la Mawaziri leo April 4, 2012
(PICHA IKULU)
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na wanahabari
 wakati wa kutangaza Baraza la Mawaziri 
leo April 4, 2012









Wanahabari wakati Rais Jakaya Mrisho Kikwete 
wakati wa kutangaza Baraza la Mawaziri leo April 4, 2012

SIMBA leo wanaanza kushangilia ubingwa wa Ligi Kuu





















SIMBA leo wanaanza kushangilia ubingwa wa Ligi 
Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baada ya Azam FC
 kufungwa mabao 2-1 na Mtibwa Sugar kwenye
 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Simba ina pointi 59, ambazo sasa haziwezi kufikiwa 
na timu yoyote msimu huu na imebakiza mechi
 moja dhidi ya watani wa jadi, Yanga Jumapili 
ambayo kwao itakuwa ya kulinda heshima tu.
 Lakini Azam tayari imejihakikishia nafasi ya pili 
kwenye ligi hiyo na hivyo kukata tiketi ya kushiriki 
Kombe la Shirikisho la Soka Afrika mwakani.
Waliokuwa mabingwa watetezi Yanga, hawana tena 
chao- kwani hata wakiifunga Simba keshokutwa 
watabaki nafasi ya tatu tu, hivyo mwakani hawavuki
 mipaka ya nchi.

Tumaini pekee la Yanga kucheza michuano ya Afrika 
mwakani ni iwapo Simba SC itaingia hatua ya makundi
 ya Kombe la Shirikisho mwaka huu- ikiwa imebakiza 
mitihani miwili kufikia mafanikio hayo.
Inatakiwa kuitoa Al Ahly Shandy ya Sudan- na baadaye
 iitoe timu itakayokutana nayo kwenye mchujo wa 
kuwania kucheza hatua hiuyo, ambayo itakuwa
 imetolewa kwenye Ligi ya Mabingwa.
Hapo, Tanzania itakuwa na nafasi mbili kwenye 
Kombe la Shirikisho mwakani, kwa mujibu wa 
anuni mpya za Shirikisho la Soka Afrika (CAF).
Tayari Simba imeifunga Shandy mabao 3-0 katika
 mchezo wa kwanza na inahitaji sare katika mchezo
 wa marudiano wiki ijayo ili kusonga mbele.

Katika mchezo wa leo, hadi mapumziko, tayari Mtibwa 
walikuwa wanaongoza kwa bao 1-0 lililowekwa kimiani 
na Awadh Issa dakika ya 25, wakati kipindi cha pili, 
Wakata Miwa hao wa Manungu waliokuwa wanashangiliwa 
kwa nguvu na mashabiki wa Simba, walipata bao la pili
 dakika ya 59, mfungaji akiwa ni Juma Abdul.

Awadh alifunga bao lake akiunganisha kona iliyochongwa
 na nyota wa mchezo wa leo, Juma Abdul ambaye naye 
alifunga bao la pili kwa mpira wa adhabu, baada ya 
Luckson Kakolaki kumchezea rafu Vencent 
Barnabas Saramba. John Raphael Bocco aliifungia
 Azam bao la kufutia machozi.

Wednesday, May 2, 2012

Don't buy Kiwis from China

 Please circulate as far as possible, everyone must be informed and they can make their own choices.
When this is being foisted on to the public without their knowledge, it is tantamount to criminal activity.
You will have noticed some unusually large Kiwi fruit on the shelves and these look very attractive too!!!

No wonder we have so many sick people when they eat products like this.


Don't buy Kiwi Fruit from China!



The Kiwi Fruit are soaked with chemicals whilst growing on trees so they will grow larger and weigh heavier.

They are using some kind of chemical growth hormones that can have bad effects upon human nervous systems including metabolic disorders, birth defects, and retarded learning abilities of children.



The Kiwi fruits, after soaking in the Chemical Hormone will grow larger and are more preferred by the merchants because they are more profitable!








Just avoid Kiwi fruit from China if you care for your family's safety!
make sure you join African social network click here to join

Sunday, April 29, 2012

Let me ask you a simple question...Could you use some extra money? You could? Great!




And if I could show you how to earn an extra 120.00USD or more per day, and all you'd need
to spend is a couple of hours a day at your home computer...

Would that intrigue you? Then read on...

Very few people know what I am going to share with you now, and those that do are
making a nice living online on social network

In fact, just normal, non-geeky people who work online earn several hundred pounds

a day doing this And no, it's not like anything else you've seen before.

You'll be shown numerous advertisement that will pay you good money to add friends view your profile  and they will be able to see ads online from you profile/

* You don't need any experience
* You don't need any special skills
* You don't need a marketing degree

All you need is a computer and internet access.

Let's face it, if these companies did all the work themselves, it would take forever! That's where you come in. Companies worldwide are bending over backwards to find people to post ads for them, and they'll pay you nicely in return.

Here's how it works.

* You invite your friend and they join get 2poits each friend who joined
* You  log in you bonglob account everyday you get points
* You choose your own hours
* You do invite friends as many as you want, no restrictions,

In fact you can start right now - today.  It's as easy as 1-2-3...

 
www.bonglob.com

* Choose the company BonGlob LTD you would like to work with
* Login to your BONGLOB.COM account.

* Sit back and wait for your cheques to come in. So if you need extra cash, act now... Go straight to


Friday, April 13, 2012

bongodar: ATAKA JAMII ISIMHUKUMU MWANAWE, HAKI ITENDEKE, AELEZA USHIRIKA WA LULU NA KANUMBA Daniel Mjema

bongodar: ATAKA JAMII ISIMHUKUMU MWANAWE, HAKI ITENDEKE, AELEZA USHIRIKA WA LULU NA KANUMBA Daniel Mjema

ATAKA JAMII ISIMHUKUMU MWANAWE, HAKI ITENDEKE, AELEZA USHIRIKA WA LULU NA KANUMBA Daniel Mjema



BABA mzazi wa msanii wa filamu, Elizabeth Michael 'Lulu,'

ATAKA JAMII ISIMHUKUMU MWANAWE, HAKI ITENDEKE, AELEZA USHIRIKA WA LULU NA KANUMBA
Daniel Mjema
BABA mzazi wa msanii wa filamu, Elizabeth Michael 'Lulu,' ameitaka jamii kutomhukumu mwanawe kutokana na kifo cha msanii mwenzake marehemu Steven Kanumba, badala yake iache vyombo vya sheria vifanye kazi yake.

Mzazi huyo, Michael Edward Kimemeta anayeishi mjini Moshi, amewaomba Watanzania kuiachia Mahakama iamue kama mtoto wao anahusika katika kifo hicho ama la.

Kimemeta, ameeleza kuwa binti yake ana umri wa miaka 16 tofauti na inavyoelezwa kuwa ana miaka 18.

Juzi Lulu alifikishwa katika Mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam na kusomewa mashtaka ya mauaji ya msanii mwenzake, Kanumba.

Kumekuwa na utata uliojitokeza kuhusu umri wa Lulu. Wakati mwenyewe akieleza kuwa ana miaka 17, Jeshi la Polisi lilieleza kuwa umri wake ni miaka 18 na juzi Mahakama iliambiwa kuwa msanii huyo ana umri wa miaka 17 na baba yake akisema ana miaka 16.

Kwa upande wake, mama mzazi wa Lulu Lucresia Karugila, alisema tukio la kifo cha Kanumba na kukamatwa kwa binti yake Lulu, limempa mshituko mkubwa na kumsababishia maradhi ya kisaikolojia na kimwili.

“Hayo yaliyotokea kwa kweli yamenifanya niumwe kabisa hapa sasa hivi nimelala naumwa…nimempa go ahead (ruksa), baba yake azungumze kwa sababu taarifa zote anazo. Naomba mimi mniache kwa sasa,”alisema.

Kimemeta aliliambia Mwananchi jana kuwa mwanawe huyo alizaliwa Aprili 17 mwaka 1995 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).

“Nataka nikuambie (mwandishi) mwanangu atatimiza umri wa miaka 17 ifikapo Aprili 17 mwaka huu. Sasa ana umri wa miaka 16 na ni mtoto. Tunavyosikia Kanumba alikuwa mpenzi wake inatuuma sana,” alisema.

Baba huyo alisema alizaa na mama yake Lulu lakini hawakuwahi kuishi pamoja. "Mwanamke huyo alikuwa akifanya kazi Shirika la Ndege Tanzania (ATC) na muda wote Lulu alikuwa akiishi na mama yake jijini Dar es Salaam,"alisema Kimemeta.

Ameomba familia ya marehemu Kanumba ikubali kupokea pole ya familia ya Lulu kupitia gazeti hili kutokana na mazingira kutoruhusu familia hizo kukutana.

“Nasikitika mazingira ya tukio lenyewe mpaka sasa hayaruhusu familia yetu kwenda kutoa pole na kuifariji familia ya Kanumba kulingana na utamaduni wa mwafrika…tunaomba wapokee pole zetu kupitia njia hii,” alisema.

Kwa mujibu wa Kimemeta, hivi sasa wanahofia maisha yao kutokana na jamii kujenga mtazamo hasi juu ya tukio hilo hata bila ya kusubiri vyombo vya sheria kusikiliza ushahidi wa tukio hilo na kutoa hukumu yake.

Alisema kuwa jamii inapaswa ifahamu kuwa, kikatiba mtu yeyote anayeshitakiwa kwa kosa lolote haimaanishi tayari ni mkosaji, bali atahesabiwa kuwa mtuhumiwa hadi pale Mahakama itakapomtia hatiani.

“Yanasemwa mengi mara ooh Kanumba ndio alianza kumpiga mwanangu mara ooh Kanumba alisukumwa …mimi nasema tuiache Mahakama hata sisi hatupendi mtu auawe, lakini Mahakama iachwe itende haki,”alisisitiza.

Akizungumzia maisha ya mwanawe Lulu, Kimemeta alisema alipokuwa akitangaza Kipindi cha Watoto Televisheni ya ITV, walifarijika sana, lakini alipoanza kuingia kwenye sanaa ya filamu, walijua sasa wamempoteza.

“Baada ya kuingia kwenye sanaa ya maigizo niliona kabisa tumempoteza mtoto na nilimweleza mama yake kuwa wale aliokuwa nao katika maigizo akiwamo Kanumba mwenyewe, nilikuwa siwaamini hata kidogo,” alisema.

Kimemeta alidai kuwa siku moja mwanawe alimpigia simu akimwarifu kuwa alikuwa anakwenda jijini Arusha kurekodi filamu na Kanumba, yeye alipinga safari hiyo akitaka Kanumba amthibitishie usalama wa binti yake.

“Kwa sababu nilikuwa sipendezwi na hayo mambo nilimwambia mama yake azungumze na Kanumba na akatuhakikishia atamlinda na kambi yake ina maadili, lakini kumbe huo ndio ukawa mwanzo wa mwanaye kugeuzwa mpenzi wa msanii huyo,”alidai.


Elizabeth Michael 'Lulu,'

Baba huyo mzazi alidai kutofanya vizuri darasani kwa mtoto wake huyo, kulichangiwa na hatua ya kuingia katika sanaa ya uigizaji.


“Lulu alikuwa mtoto mwenye tabia nzuri sana hata alipokuwa ITV kwa kweli alitutia moyo wazazi wake kwa jinsi ITV walivyokuwa wakimlea, lakini alipojiingiza tu kwenye uingizaji hapo ndipo mambo yalipoharibika,” alisema.

Alikanusha madai kuwa mwanawe hakumaliza kidato cha nne na kusisitiza kuwa Lulu alisoma Shule ya Kimataifa ya St Mary's na baadaye alihamia Shule ya Sekondari ya Midway High School na kumaliza kidato cha nne mwaka jana.

Alisisitiza kuwa katika mambo yaliyokuwa yakiwaumiza mioyo, ni namna mtoto huyo alivyozidi kuharibika kwa kuingia katika fani ya uigizaji filamu.

Alisema angependa kukutana na Rais Jakaya Kikwete ili azungumze naye kama rafiki yake na watafute suluhisho la maadili kwa kizazi cha sasa na cha baadaye.

Alisema tayari ameanza mchakato wa kuonana na Rais Kikwete ili amweleze siri aliyodai ni ‘nzito’ na kudai tayari ametafuta wazee watatu wenye busara wa kumsindikiza, endapo Rais atakubali ombi lake.

Pia ameziomba taasisi zinazojishughulisha na masuala ya haki za binadamu na msaada wa kisheria, kujitokeza na kumsaidia mwanawe.

Lulu alifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam juzi na kusomewa shitaka la kumuua
Kanumba, tukio lililotokea Aprili 7 mwaka huu eneo la Sinza Vatican.

Msanii huyo hakutakiwa kujibu lolote kwa kuwa Mahakama hiyo haina
mamlaka ya kusikiliza mashauri ya mauaji na hivyo alipelekwa rumande Gegeza la Segerea hadi Aprili 23 mwaka wakati kesi hiyo itakapotajwa.

Kifo cha msanii huyo kimetikisa nchi kutokana na umaarufu wake, akiwa ameigiza filamu 40 zilikuwa zikirushwa katika vituo mbalimbali vya
televisheni ndani na nje ya nchi.


Kanumba alipanga kujenga shule

Katika hatua nyingine, Fidelis Butahe na Pamela Chilongola wanaripoti kuwa mchaguaji maeneo ya kupigia picha za filamu za msanii Kanumba, Rahim Khatib alisema marehemu Kanumba alinunua eneo la ekari 15 huko Mpiji mkoani Pwani kwa ajili ya ujenzi wa shule yake ya sekondari.

Khatib alisema Kanumba alikuwa na mpango huo muda mrefu na kwamba lengo lake lilikuwa kuwasaidia wanafunzi wa eneo hilo ambao hutembea muda mrefu kutokana na shule kuwa mbali na eneo hilo.

“Kanumba alikuwa na mipango mizuri katika maisha yake, kuna eneo kubwa alilonunua Mpiji ili ajenge shule ya sekondari,” alisema Khatib.

Alifafanua kuwa hadi anafariki dunia, aliacha kiasi cha fedha zaidi ya Sh 40 milioni katika Kampuni yake ya Kanumba The Great.

“Marehemu ameacha fedha zaidi ya Sh 40 katika kampuni yake, magari matatu na hivi karibuni alinunua jingine aina ya Toyota Land Cruiser, ”alisema Khatib.

Katika hatua nyingine Khatib alisema kifo cha Kanumba ni pigo kwa watu waliokuwa wakifanya naye kazi akiwemo yeye mwenyewe kwa kuwa walikuwa wakimtegemea kwa kiwango kikubwa.

Sintah naye alonga

Kwa upande wake msanii maarufu wa filamu nchini, Christina Manongi maarufu kama Sintah ambaye alikuwa mmoja wa wasanii wa kwanza kufika nyumbani kwa marehemu Kanumba muda mfupi baada ya msanii huyo kuanguka, alisema kuwa siku tano kabla ya Kanumba kufariki, alikuwa na hasira tofauti na alivyomzoea.

Sintah ambaye alikuwa na msanii huyo katika Viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam Jumapili ya Aprili mosi pamoja na mwigizaji mwingine, Steve Nyerere alisema kuwa kila alichokuwa akimuuliza Kanumba, alimjibu kwa ukali.

“Ni tofauti na nilivyomzoea, siku ile ya Jumapili tulikaa pale Leaders Club mpaka usiku sana na kila jambo nililokuwa nikizungumza naye alinijibu kwa mkato na ukali kweli, ilinishangaza,” alisema Sintah

Alifafanua kuwa moja ya mambo waliyokuwa wakizungumza na Kanumba ni pamoja na yeye kutaka kuacha uigizaji, suala ambalo marehemu Kanumba hakuliunga mkono na kumjibu kwa ukali kuwa asijitoe katika uigizaji.